Matthew 5:3-12
3“Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao.b
4Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa.c
5Heri walio wapole, maana watairithi nchi.d
6Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo Mungu, maana watashibishwa.e
7Heri walio na huruma, maana watahurumiwa.f
8Heri wenye moyo safi, maana watamwona Mungu.g
9Heri wenye kuleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu.h
10Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana ufalme wa mbinguni ni wao.i
11“Heri yenu ninyi watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa ajili yangu.j
12Furahini na kushangilia maana tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Hivyo ndivyo walivyowadhulumu manabii waliokuwako kabla yenu.k